MWANI

21 Sep, 2022 - Sea Moss

Hivi karibuni  zao la Mwani Tanzania limekua na soko kubwa kutokana na selikali kutoa elimu kwa wananchi umuhimu wa kutumia vyakula asili, mfumo wa maisha wa sasa umebadirika magonjwa yamekua mengi na mapya kila kukicha tujifunze  kusoma tafiti mbali mbali za wataalamu wa afya. Tujifunze kupandisha kinga za mwili hasa kwa kuzingatia vyakula asilia, mboga mboga na matunda.
Tunapaswa kufahamu   Pia kujifunza Na kulinda afya zetu.

MWANI
sea moss ni aina ya mimea inayoota na kukua kwenye maji chumvi (bahari)
Sea moss hautegemei mizizi kufyonza maji na virutubisho vingine bali hutumia sehemu zote za mmea kufyonza virutubisho vinavohitajika kutoka kwenye maji.

Mwani unaposindikwa, hutoa ute(gel) hutumika  kwenye viwanda kama 
•usindikaji wa vyakula,
•vinywaji, 
•Rangi za kupaka, 
•dawa za meno, 
•sabuni, 
•shampoo n.k
Kwa wajasilia Mali na wale ambao bado hawajajiajili ila wanaopenda kujiajili Leo nimewafungulia mlango, Hii ni fursa kubwa sana kwenu 
Mwani  ni marighafi nzurii na kwa sasa inakubarika  sokoni kwa kutoa bidhaa nzurii zenye ubora.
Pia mmea huu   hutumika kama chakula dawa

Mwani una  vitamins na madini 92 kati ya madini 110 ambayo mwili umejengwa nayo. (Sea moss ni kama Supplement)

Mwani hutimika pia kutengeneza Chakula cha
wanyama na kutengeneza mbolea.

FAIDA ZA SEA MOSS (mwani)
Mwani huongeza ukuaji wa bakteria nzuri na kulisha utumbo.

Seamoss ina sifa za antiviral & anti microbial ambayo husaidia katika kuondoa kila aina ya maambukizi. Hivyo inaboresha kinga ya mwili.

Seamoss ina potassium chloride,ambayo husaidia mwili kupunguza uvimbe. Na watu hutumia ili kupunguza athari za maambukizi kwa sababu ya nguvu yake ktk kinga ya mwili.

Seamoss ina utajiri wa madini aina ya folate ambayo ni ufunguo katika ukuaji wa kichanga tumboni, hivyo ni muhimu kwa mama mjamzito.

Seamoss ni laxative ( kwa kiwango kidogo ) Ila  yenye ufanisi!  Hii inamaanisha hakuna kuvimbiwa tena! . Husafisha colon ( utumbo mkubwa)kwa ufanisi pia Hupunguza tishu zilizowaka kwenye mfereji  wa tumbo.

Seamoss ina utajiri wa madini ya zinc ambayo Husaidia Libido na huboresha utendaji wa tendo la ndoa. Seamoss hutambulika kama viagra ya asili.

-Huchochea seli kupata hewa ya Oxygen
-Huboresha ufyonzaji wa virutubisho
-Huimarisha mifupa
-Hunuisha ngozi/ nywele/kucha -Huongeza kinga mwilini -Hupunguza uvimbe
-Huondoa kamasi katika mwili -Hupambana uzee (anti-aging) -huongeza nishati. ( energy) 
- inaimarisha kazi ya Thyroid -Hupunguza maumivu ya viungio ( joints) 
-Afya ya moyo
-Nzuri kwa lishe
-Nzuri kwa afya ya uzazi 
-Husaidia kupambana na maambukizi mbalimbali.
-Afya ya mapafu
-afya ya akili na hata mwili kiujumla -Afya ya mwanamke
-Huboresha tendo la ndoa -Husaidia matatizo ya allergy mbalimbali
-husaidia kutatua shida za usingizi.

Seamoss ikiandaliwa katika mfumo wa gel ( jelly) inaweza wekwa katika juice/smoothie, chai pendwa, soup au hata maji moto. Ila zaidi ya yote hutumika yenyewe kama yenyewe.

Matumizi yake huwa kuanzia vijiko 2-3 kwa siku ( japo hauna kikomo katika matumizi) kwani hauhesabiki kama dawa bali kama chakula ( superfood).

SEA MOSS GEL
jinsi ya kutengeneza
Chukua Mwani mkavu osha vizuri kutoa michanga , harufu, na chumvi

Loweka kamulia  ndimu ya tunda acha humo na maganda yake kwenye maji masafi ya kawaida, kwa mda kuanzia masaa 12....hadi iwe Laini vizuri Kisha  Saga kwenye blenda  iwe kama uji mzito hifadhi vizuri kwenye fridge tayar kwa matumizi.

Matumizi
Tumia kijiko 1-2kwa ck
ukichanganya kwenye kila mlo wako  kama vile :
supu, juice, kachumbari n.k
lakin pia unaweza kutumia fresh bila kuchanganya kwenywe chakula

Mtoto unampa Kijiko 1